Real Madrid wanamtaka nahodha wa Chelsea Reece James lakini The Blues watadai ada kubwa kwa beki huyo wa England mwenye umri wa miaka 23. (Teamtalk)
AC Milan wana nia ya kumsajili beki Mwingereza Lloyd Kelly mwenye umri wa miaka 25 kutoka Bournemouth, ingawa Tottenham pia wanamnyatia. (Tuttosport - usajili unahitajika, kwa Kiitaliano)
Juventus, Borussia Dortmund, Fulham na West Ham United ni miongoni mwa klabu zingine zinazomtaka Kelly, ambaye mkataba wake unaisha msimu ujao. (90 min)
Arsenal huenda wakamnunua kiungo wa kati wa Royal Antwerp Arthur Vermeeren kwa pauni milioni 13 mwezi Januari, lakini Barcelona pia wanamtaka mchezaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 18. (Sport - kwa Kihispania)
Manchester United wanatafuta mbadala wa kocha Erik ten Hag, huku meneja wa Sporting Lisbon Ruben Amorim na mkufunzi wa zamani wa Real Madrid Zinedine Zidane wakipigiwa upatu kuchukua nafasi yake. (Times - usajili unahitajika)
Manchester United wanataka kumsajili mshambuliaji mwingine ili kumuunga mkono Mdenmark Rasmus Hojlund huku wasiwasi ukiongezeka kuhusu maendeleo ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 20. (Mail)
Ivan Toney wa Brentford ni chaguo mojawapo linaloangaliwa na Ten Hag, pamoja na mshambuliaji wa Napoli na Nigeria Victor Osimhen, 24, na mshambuliaji wa Iran na Porto Mehdi Taremi, 31. (Express)
Mshambuliaji wa Uingereza Toney ameithibitishia Brentford kwamba angependa kuondoka mara tu dirisha la usajili la Januari litakapofunguliwa, huku Arsenal na Chelsea wakiripotiwa kutaka kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (90min)
Everton wako kwenye mazungumzo na Tottenham kuhusu kubadilisha makubaliano ya uhamisho wa kiungo wa Uingereza Dele Alli, 27. Watakuwa na deni la Spurs la pauni milioni 10 ikiwa Alli atacheza mechi saba zaidi. (Mirror)
Manchester United wanaweza kumnunua kipa wa Porto na Ureno Diogo Costa, 24, huku Andre Onana wa Cameroon akitarajiwa akashiriki Kombe la Mataifa ya Afrika. (Todo Fichajes - kwa Kihispania)
Mshambuliaji wa England Eberechi Eze, 25, ataongeza mshahara wake mara tatu kwa kandarasi mpya ya Crystal Palace ambayo itakuwa na kipengele kikubwa cha kuachiwa. (Teamtalk)
Beki wa Aston Villa na Uhispania Pau Torres, 26, anasema alikuwa karibu kujiunga na Real Madrid kutoka klabu ya zamani ya Villarreal msimu wa 2021. (Sky Sports).
Barcelona wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Bayern Munich na Ujerumani Joshua Kimmich huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28 akiwa hana matumaini kusaini mkataba mpya na klabu hiyo ya Ujerumani. (Fichajes - kwa Kihispania)
BBC