Simba - Yanga - Local

Bodi ya Ligi yawahakikishia mashabiki usalama Jumapili

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 Nov 2023
Bodi ya Ligi yawahakikishia mashabiki usalama Jumapili

Bodi ya Ligi Kuu (TPLB) imewahakikishia mashabiki wote watakaoingia uwanja wa Benjamin Mkapa kushuhudia mchezo wa dabi ya Kariakoo kati ya Simba dhidi ya Yanga siku ya Jumapili, usalama utakuwa wa kutosha

Aidha, TPLB imewataka mashabiki wanaokwenda na silaha uwanjani kuzisalimisha kituo cha polisi kilicho karibu na uwanja huo na baada ya mechi watafuata silaha zao

Kauli hiyo imetolewa na Afisa Habari wa TPLB, Karim Boimanda wakati akizungumzia maandalizi kuelekea mchezo huo utakaopigwa Jumapili, Novemba 05 saa 11 jioni

"Kuna mashabiki wanaingia na silaha uwanjani, hivyo kwa yeyote anayemiliki silaha na anatembea nayo basi siku hiyo atalazimika kuacha kituo cha Polisi maana hataruhusiwa kuingia nayo"

"Mashabiki watakaguliwa, maana kule ndani usalama utakuwepo wa kutosha kutoka Jeshi la Polisi," alisema Boimanda

Boimanda amesema mageti siku hiyo yatafunguliwa kuanzia saa 4:00 asubuhi hivyo amewataka mashabiki kukata tiketi mapema ili kuepuka usufumbufu na wale watakaopewa mialiko maalumu kuhakikisha hawagawi mialiko yao kwa mtu mwingine.

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
4h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
4h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
4h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
8h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
11h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
12h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
12h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
13h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
14h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
15h ago
READ MORE β†’