Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira ametwaa tuzo ya kocha bora wa ligi kuu ya NBC kwa mwezi Oktoba 2023
Robertinho ametwaa tuzo hiyo baada ya kuiongoza Simba kushinda mechi zote tatu zilizochezwa katika mwezi Oktoba
Ametwaa tuzo hiyo akiwashinda kocha wa KMC Abdulhamad Moalin na Miguel Gamondi wa Yanga

Katika mwezi Oktoba Robertinho aliiongoza Simba kushinda mechi dhidi ya Prisons, Singida BS na Ihefu Fc
Nae kiungo mshambuliaji wa Yanga Stephane Aziz Ki ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Oktoba 2023 Ligi Kuu ya NBC
Aziz Ki ameshinda tuzo hiyo baada ya kufunga mabao manne katika mechi za ligi kuu walizocheza Yanga mwezi Oktoba
Ki alichuana na Maxi Nzengeli na Moses Phiri wa Simba

Tuzo ya Meneja bora wa mwezi ilikwenda kwa Malule Omar, Meneja wa uwanja wa Highland Estates, Mbarali



