Robertinho, Aziz Ki washinda tuzo Ligi Kuu Oktoba

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd November 2023


Robertinho, Aziz Ki washinda tuzo Ligi Kuu Oktoba

Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira ametwaa tuzo ya kocha bora wa ligi kuu ya NBC kwa mwezi Oktoba 2023

Robertinho ametwaa tuzo hiyo baada ya kuiongoza Simba kushinda mechi zote tatu zilizochezwa katika mwezi Oktoba

Ametwaa tuzo hiyo akiwashinda kocha wa KMC Abdulhamad Moalin na Miguel Gamondi wa Yanga

Katika mwezi Oktoba Robertinho aliiongoza Simba kushinda mechi dhidi ya Prisons, Singida BS na Ihefu Fc

Nae kiungo mshambuliaji wa Yanga Stephane Aziz Ki ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Oktoba 2023 Ligi Kuu ya NBC

Aziz Ki ameshinda tuzo hiyo baada ya kufunga mabao manne katika mechi za ligi kuu walizocheza Yanga mwezi Oktoba

Ki alichuana na Maxi Nzengeli na Moses Phiri wa Simba

Tuzo ya Meneja bora wa mwezi ilikwenda kwa Malule Omar, Meneja wa uwanja wa Highland Estates, Mbarali


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.