Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema kikosi chake kinazihitaji alama zote tatu katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Yanga ambao utapigwa kesho Jumapili kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa
Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo, Robertinho amesema anatambua mchezo huo hautakuwa mwepesi kwa sababu ni derby lakini jambo muhimu kwa kikosi chake ni kucheza vizuri na kupata ushindi
"Falsafa yangu kwenye mpira wa miguu ni kucheza vizuri na kushinda mechi, Nawaheshimu Yanga ni timu nzuri, lakini nina imani kubwa na wachezaji wetu pamoja na maandalizi mazuri tuliyofanya"
"Mechi ya Derby siku zote haitabiriki. Derby inaamuliwa baada ya dakika 90 za mchezo, tunaiheshimu Yanga lakini tutaingia kwenye mchezo kwa lengo la kutafuta pointi tatu"
"Ninawaamini wachezaji wangu, wana vipaji vikubwa na tumejipanga kushinda. Sina presha ya mechi ya kesho, ni kama michezo mingine lakini kupata pointi tatu ndicho kipaumbele chetu," alisema Robertinho
Simba inazihitaji alama tatu za mchezo dhidi ya Yanga ili kujiweka katika nafsi nzuri zaidi kwenye mbio za ubingwa
Kimahesabu Simba ina nafasi ya kuongoza ligi kwa tofauti ya alama sita kama itashinda mchezo dhidi ya Yanga kesho na mchezo wa kiporo dhidi ya Mashujaa