Simba hoi mbele ya Yanga, yapigwa 5G

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th November 2023


Simba hoi mbele ya Yanga, yapigwa 5G

Rekodi imeandikwa uwanja wa Benjamin Mkapa leo 5G ikirejea tena  mitaa ya Twiga na Jangwani

Ulichoona hapo juu hujakosea! Yanga imeibuka na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Simba

Ilikuwa suala la muda tu, ubora wa Yanga ukadhihiri kwenye kipindi cha pili Wananchi wakifunga mabao manne baada ya sare ya 1-1 mpaka wakati wa mapumziko

Kennedy Musonda aliitanguliza Yanga kwa bao safi la kichwa kwenye dakika ya tatu akimalizia krosi ya Yao Kouassi

Simba walirejesha bao hilo dakika chache baadae kwa mpira wa kichwa kutoka kwa Kibu Denis

Lakini shughuli waliyokutana nayo Simba kwenye kipindi cha pili kwa hakika hawatakuja kusahau maisha mwao

Maxi Nzengeli aliweka kambani bao la pili baada ya pasi ya Aziz Ki kabla ya Aziz Ki kufunga la tatu akipokea pasi ya Clement Mzize aliyengia kwenye kipindi cha pili na kubadili taswira ya mchezo

Alikuwa Mzize tena aliyetengeneza bao la nne lililofungwa na Nzengeli kabla ya Pacome Zouzoua kufunga la tano baada ya Nzengeli kuangushwa kwenye eneo la hatari

Yanga imerejea kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 21


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.