Rekodi imeandikwa uwanja wa Benjamin Mkapa leo 5G ikirejea tena mitaa ya Twiga na Jangwani
Ulichoona hapo juu hujakosea! Yanga imeibuka na ushindi wa mabao 5-1 dhidi ya Simba
Ilikuwa suala la muda tu, ubora wa Yanga ukadhihiri kwenye kipindi cha pili Wananchi wakifunga mabao manne baada ya sare ya 1-1 mpaka wakati wa mapumziko
Kennedy Musonda aliitanguliza Yanga kwa bao safi la kichwa kwenye dakika ya tatu akimalizia krosi ya Yao Kouassi
Simba walirejesha bao hilo dakika chache baadae kwa mpira wa kichwa kutoka kwa Kibu Denis
Lakini shughuli waliyokutana nayo Simba kwenye kipindi cha pili kwa hakika hawatakuja kusahau maisha mwao
Maxi Nzengeli aliweka kambani bao la pili baada ya pasi ya Aziz Ki kabla ya Aziz Ki kufunga la tatu akipokea pasi ya Clement Mzize aliyengia kwenye kipindi cha pili na kubadili taswira ya mchezo
Alikuwa Mzize tena aliyetengeneza bao la nne lililofungwa na Nzengeli kabla ya Pacome Zouzoua kufunga la tano baada ya Nzengeli kuangushwa kwenye eneo la hatari
Yanga imerejea kileleni mwa msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 21







