Simba - Local

Simba yatuliza mashabiki baada ya kipigo

Joel JJ By Joel JJ
6 Nov 2023
Simba yatuliza mashabiki baada ya kipigo

Uongozi wa klabu ya Simba umewaomba radhi mashabiki baada ya kupoteza mchezo wa watani wa jadi dhidi ya Yanga uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa jana

Aidha Simba imewashukuru mashabiki kwa kujitokeza kwa wingi katika mchezo huo ambao ulimalizika kwa Simba waliokuwa wenyeji kufungwa mabao 5-1

Meneja wa Habari na Mawasiliano Ahmed Ally amesema ni maumivu makali kila Mwanasimba anapitia baada ya kipigo hicho

Maumivu hayo yatadumu kwa muda mrefu kwani matokeo hayo tayari yameingia katika vitabu vya kumbukumbu

Hata hivyo jambo la msingi ni kuwa mchezo huo umepita, kila sehemu yenye mapungufu imeonekana libaki kuwa jukumu la uongozi, benchi la ufundi na wachezaji kusahihisha

Haupaswi kuwa wakati wa kulaumiana kwani kuna mechi nyingine ya Ligi Kuu inafuata siku chache zijazo dhidi ya Namungo Fc (Alhamisi) na huu ni mchezo ambao Simba inahitaji kushinda

"Kwenye Mkutano wa Wanahabari nilisema, Hii ni mechi ambayo matokeo yake hua yanaacha furaha ya kudumu au huacha maumivu ya kudumu kwenye mioyo ya mashabiki wake"

"Bahati mbaya ni sisi ndo tunabaki na maumivu ya kudumu Kila Mwana Simba anawaza sababu tafauti tofauti iliyosababisha tupoteze mchezo wa jana"

"Iko namna sahihi ya kujua sababu hizo nayo ni utulivu.Tuwape viongozi, benchi la ufundi na wachezaji wetu utulivu wa kujitathmini kwa maslahi ya mechi zijazo"

"November 9 kuna mchezo dhidi ya Namungo hivyo ni vema tukajikita zaidi kuangalia tunachukuaje alama tatu hizo baada ya kupoteza jana," alisema Ahmed

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
12h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
13h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
15h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
15h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
16h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
16h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
17h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
17h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
17h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
19h ago
READ MORE →