JKT Queens yaanza kwa kipigo Ligi ya Mabingwa Wanawake

Joel JJ By Joel JJ β€’ 6th November 2023


JKT Queens yaanza kwa kipigo Ligi ya Mabingwa Wanawake

JKT Queens imeanza vibaya michuano ya Ligi ya Mabingwa ya Wanawake baada ya kupokea kichapo cha mabao 2-0 dhidi ya Mamelodi Sundowns kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi uliochezwa jana Uwanja wa Amadou Gon Coulibaly, Ivory Coast

Mabao la Mamelodi yamefungwa na Lebohang Ramal dakika ya 40 ya mchezo na kipindi cha pili wakapata bao la pili dakika ya 74 Refilwe Tholakele 75.

Mchezo huu ni wa kwanza kwa JKT Queens kukutana na Mamelodi na pia hii inakuwa mara ya pili kwa timu za Tanzania kushiriki michuano hiyo baada ya msimu uliopita Simba Queens kuchukua ubingwa wa CECAFA na kuishia nusu fainali CAF

JKT Queens walipata nafasi ya kushiriki michuano hiyo baada ya kuwa mabingwa wa soka la Wanawake Tanzania na pia kutwaa taji la CECAFA ambalo liliwapa tiketi ya kwenda Ivory Coast


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.