JKT Queens imeanza vibaya michuano ya Ligi ya Mabingwa ya Wanawake baada ya kupokea kichapo cha mabao 2-0 dhidi ya Mamelodi Sundowns kwenye mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi uliochezwa jana Uwanja wa Amadou Gon Coulibaly, Ivory Coast
Mabao la Mamelodi yamefungwa na Lebohang Ramal dakika ya 40 ya mchezo na kipindi cha pili wakapata bao la pili dakika ya 74 Refilwe Tholakele 75.
Mchezo huu ni wa kwanza kwa JKT Queens kukutana na Mamelodi na pia hii inakuwa mara ya pili kwa timu za Tanzania kushiriki michuano hiyo baada ya msimu uliopita Simba Queens kuchukua ubingwa wa CECAFA na kuishia nusu fainali CAF
JKT Queens walipata nafasi ya kushiriki michuano hiyo baada ya kuwa mabingwa wa soka la Wanawake Tanzania na pia kutwaa taji la CECAFA ambalo liliwapa tiketi ya kwenda Ivory Coast



