Baada ya mchezo dhidi ya Yanga ambao ulimalizika kwa kipigo cha aibu cha mabao 5-1, uongozi wa Simba umekuwa kimya lakini huenda wakaibuka na mshindo mkubwa
Baadhi ya viongozi wenye ushawishi kwenye Bodi, wameomba Bodi ikutane kwa dharura kujadili na kuamua juu ya hatma ya Kocha Robertinho Oliveira na benchi lake la ufundi
Kumekuwa na maoni tofauti baada ya mchezo dhidi ya Yanga, ukweli ni kuwa viongozi wa Simba pia wameumizwa sana na matokeo hayo, kiuhalisia hakuna aliyetarajia kama yangetokea
Kocha Robertinho ndiye aliyeteka mijadala kila kona baadhi wakitaka aondolewe huku wengine wakipendekeza Kocha Juma Mgunda aongezwe kwenye benchi la ufundi ili wasaidiane
Simba inaelekea kwenye hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa, ipo hofu kama itaweza kufanya vizuri katika michuano hiyo kwa kuangalia mwenendo wake msimu huu katika mechi za Kimataifa
Msimu huu Simba imepata sare mechi zote za Kimataifa kuanzia raundi ya kwanza ligi ya mabingwa dhidi ya Power Dynamos na mechi mbili za AFL dhidi ya Al Ahly



