Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Novemba 08 2023

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th November 2023


Tetesi za soka Ulaya, Jumatano Novemba 08 2023

Manchester United wana nia ya kumsajili beki wa kati wa Nice Jean-Clair Todibo, 23, kama mbadala wa mchezaji wa kimataifa Raphael Varane, 30, ambaye anaweza kuelekea Saudi Arabia. (caught offside)

Bournemouth itakataa mbinu zozote za kumnunua mlinzi Lloyd Kelly mwezi Januari, huku Tottenham, Liverpool, Newcastle na AC Milan zikiwa na nia ya kumnunua Mwingereza huyo mwenye umri wa miaka 25. (Teamtalk)

Wakala wa mlinzi wa Manchester United Mbrazil Antony, 23, anasema mteja wake hatarejea katika nchi yake kwa makubaliano ya kubadilishana mshambuliaji mwenye umri wa miaka 27, Gabriel Barbosa kutoka Flamengo. (Jorge Nicola, via Express)

Miamba wa Italia Juventus wanavutiwa na mkataba wa mkopo wa kiungo wa kati wa Uingereza Kalvin Phillips, 27, ambaye anaelekea kuondoka Manchester City mwezi Januari. (Team talk)

Kiungo wa kati wa Liverpool Thiago Alcantara, 32, analengwa na klabu za Serie A, Juventus na Inter Milan, huku mkataba wa mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania na Reds ukimalizika mwishoni mwa msimu huu. (Fichajes)

Kiungo wa kati wa Italia Manuel Locatelli, 25, anatazamiwa kusaini mkataba mpya na Juventus hadi Juni 2028. (Fabrizio Romano)

Chelsea na Liverpool wana nia ya kumsajili mlinzi wa Real Betis mwenye umri wa miaka 18 Assane Diao. (Mucho Deporte, via Football Talk)

Chelsea na Manchester United watalazimika kutumia euro 50m (£43m) kama wanataka kumsajili beki wa kulia wa Uholanzi Denzel Dumfries, 27, kutoka klabu ya Italia Inter Milan. (CalcioMercato)

Arsenal, Fulham na Liverpool zilituma wawakilishi kumtazama kiungo wa Fluminense Andre wakati wa fainali ya Copa Libertadores. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil mwenye umri wa miaka 22 ana makubaliano ya kuondoka kwa mabingwa hao wa Amerika Kusini, ambao thamani yake ni euro 35m (£30.4m) mwezi Januari. (Globo Esporte)

Mlinzi wa Uhispania Marco Alonso, 32, anatarajiwa kuondoka Barcelona na kwenda kwa wapinzani wa La Liga Atletico Madrid. (Football Transfers)

BBC


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.