Yanga yaichapa Coastal Union 1-0

Joel JJ By Joel JJ β€’ 8th November 2023


Yanga yaichapa Coastal Union 1-0

Bao la dakika ya 71 lililofungwa na Clement Mzize limeihakikishia Yanga alama tatu muhimu mkoani Tanga katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Coastal Union

Krosi ya Jesus Moloko aliyeingia kipindi cha pili ilitumiwa vyema na Mzize aliyeweka mpira kimiani kwa kichwa

Ilikuwa mechi ngumu, ikumbukwe ni siku tatu tu zimepita tangu Yanga ichuane na Simba uwanja wa Benjamin Mkapa na Wananchi kuibuka na ushindi wa mabao 5-1

Ni aina ya mechi ambazo alama tatu ndio matokeo muhimu zaidi ambayo Wananchi watafurahia lakini walipata upinzani kutoka Coastal Union iliyoingia na mkakati wa kujilinda zaidi

Alama 24 kibindoni Yanga ikizidi kupaa kileleni mwa msimamo wa Ligi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.