Mlinda lango wa Yanga Aboutwalib Mshery jana alirejea uwanjani baada ya kukosekana kwa takribani miezi tisa
Mshery alidaka dakika zote 90 za mchezo wa ligi kuu dhidi ya Coastal Union uliopigwa uwanja wa Mkwakwani Yanga ikiibuka na ushindi wa bao 1-0
Mshery amesema sasa yuko fit kwa asilimia 100% kuipambania Yanga na timu ya Taifa
"Takribani miezi tisa bila mechi yoyote ya ushindani na haikuwa rahisi mpaka kufikia hapa nilipo sasa. Alhdulilah sasa hivi nipo fiti na nipo Tayari kuipambania bendera ya nchi yangu na nembo ya timu yangu, Yanga," aliandika Mshery kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii
Mshery ni miongoni mwa wachezaji walioitwa kuunda kikosi cha Taifa Stars kwa ajili ya mechi za kuwania kufuzu kombe la Dunia 2026
Stars itacheza mechi mbili dhidi ya Niger na Morocco



