Simba imeshindwa kuondoka na alama zote tatu kwenye uwanja wa Uhuru baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Namungo FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC
Namungo Fc walikuwa wa kwanza kufunga bao la uongozi kwenye dakika ya 29 kupitia kwa Reliants Lusajo aliyetumia vyema makosa ya safu ya ulinzi ya Simba
Hata hivyo Simba ilirejea na kasi kubwa kwenye kipindi cha pili na kufanikiwa kusawazisha bao hilo kupitia Jean Baleke
Baleke amefikisha mabao saba sawa na Maxi Nzengeli na Stephane Aziz Ki wote wa Yanga
Huo ulikuwa mchezo wa kwanza kwa Simba tangu wamtimue aliyekuwa kocha wao mkuu Robertinho Oliveira