Klabu ya Mamelodi Sundowns imekuwa bingwa wa michuano ya African Football League (AFL) 2023 ikiwa ni mara ya kwanza kufanyika kwake
Mamelodi imeshinda kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-2 katika fainali iliyoanza kuchezwa Novemba 5 Morocco na wenyeji Wydad kushinda 2-1 na leo Novemba 12 imefikia tamati kwa Mamelodi kushinda 2-0 na kujihakikishia kitita cha Sh9.9 bilioni
Michuano hiyo ilizinduliwa Oktoba 20 jijini Dar es Salaam kwa mechi ya Simba vs Al Ahly
Timu zilizoshiriki ni Simba, TP Mazembe, Al Ahly, Wydad Casablanca, Enyimba, Esperance, Petroleos de Luanda na Mamelodi Sundowns
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi klabu ya Simba Salim Abdallah 'Try Again' ni miongoni mwa wageni mashuhuri walioshuhudia hitimisho la michuano hiyo



