Simba kushusha kocha wiki hii

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th November 2023


Simba kushusha kocha wiki hii

Baada ya mapumziko ya siku chache, kikosi cha Simba kimerejea mazoezini leo kuanza maandalizi ya mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika dhidi ya Asec Mimosas

Mchezo huo utapigwa Novemba 25 katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam

Simba imerejea mazoezini ikiwa bado iko chini ya Kaimu Kocha Mkuu Daniel Cadena na Kocha Msaidizi Seleman Matola wakati mabosi wa Simba wakiendelea na mchakato wa kusaka kocha mpya

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ally amesema wiki hii watamtambulisha Kocha Mpya ambaye atakuja na kocha msaidizi

"Tunakamilisha mchakato wa kupata kocha mpya, sio muda mrefu tutamtambulisha sambamba na kocha msaidizi. Tunatarajia ataiandaa timu kuelekea mchezo dhidi ya Asec Mimosas," alisema Ahmed

Simba imeweka malengo ya angalau kutinga nusu fainali ya ligi ya mabingwa ikiwa kundi B sambamba na Asec, Jwaneng na Wydad


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.