Azam Fc kujipima Kenya

Joel JJ By Joel JJ β€’ 14th November 2023


Azam Fc kujipima Kenya

Azam FC itasafiri nchini Kenya ambapo inatarajia kucheza mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Kenya (FKF-PL), Gor Mahia, jijini Nairobi, Novemba 19

Azam inakwenda kucheza mechi hiyo ikiwa ni moja ya maandalizi ya mchezo ujao wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar utakaochezwa Novemba 24, kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam

Ofisa Habari wa Azam FC, Thabit Zacharia 'Zaka Zakazi’' ametaja sababu ya timu hiyo kusafiri nchini Kenya

"Unajua timu zote ambazo tungetaka kucheza nazo hapa ni zilezile tunazokutana nazo kwenye ligi, hivyo kusingekuwepo na tofauti yoyote ndiyo maana tumeona tucheze na Gor Mahia mechi ambayo itakuwa na tofauti kubwa"

"Timu itaondoka Novemba 18, siku itakayofuata tutacheza mechi na baada ya mechi tutarudi (nchini) kuendelea na maandalizi ya mwisho ya kucheza na Mtibwa Sugar," alisema


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.