Yanga yasambaza mabango ya 5G Dar

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th November 2023


Yanga yasambaza mabango ya 5G Dar

Licha ya kutishiwa kushitakiwa na watani zao Simba kwa kutumia logo yao kwenye mabango ya ushindi wa mabao 5-1 ambayo Yanga wanayasimika kwenye mitaa ya jiji la Dar es salaam, Wananchi wameendelea kusimika mabango hayo ya 5G

Mkurugenzi wa Sheria wa Yanga Simon Patrick ametoa ufafanuzi ambapo amesema jambo kubwa la kwanza lililofanywa na Yanga kupitia mabango hayo ni kufurahia ushindi wao dhidi ya watani zao lakini pia kutambua thamani ya Wadhamini wao na hivyo kufungua mlango wa fursa kwa Wadhamini zaidi kujitokeza kuweka fedha zao Yanga

"Wakati watu wengi wanaona 5G kwenye bango, sisi tunatambua mchango na thamani ya wadhamini wetu ambao ni @tzsportpesa @gsmgroupofcompanies @haiertanzania @azamtvtz na @nic_insurance"

"Wadhamini hawa wameendelea kuifanya Yanga itambe na kusimika mimara ya 5G toka ligi ianze, tunatumia fursa hii kuwaalika wadhamini wengine ambao wangependa kudhamini 5G zinazokuja ndo muda sasa wa kuchangamkia fursa"

"Tuendelee kupiga picha kwenye bando, kisha kuzipost huku ukiutag ukurasa rasmi wa @yangasc ili ujishindie zawadi nono," aliandika Simon kwenye ukurasa wake wa mtandao wa kijamii

Mwenyekiti wa zamani klabu ya Simba Ismail Aden Rage amewashauri Wanasheria wa klabu hiyo kuchukua hatua ya kudai fidia kwa nembo ya Simba kutumika katika mabango hayo yenye mtazamo wa kibiashara


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.