Kocha wa zamani wa Simba Sven Vandenbroeck amesema yuko tayari kuchukua majukumu yaliyoachwa na Robertinho Oliveira
Sven aliyeinoa Simba misimu miwili iliyopita na kuisaidia kushinda mataji yote ya ndani na kuipeleka hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa, ametoa kauli hiyo katika mahojiano maalum na mtandao wa iDiski Times, Afrika Kusini
Sven amesema anaifahamu vyema Simba na anafahamu utamaduni wa klabu, ari ya mashabiki ambao wanaipenda sana klabu yao
Aidha Sven akaeleza sababu ya kutodumu katika klabu alizozifundisha nchini Morocco na Algeria sasa akiwa hana timu
"Kimsingi niko tayari kurejea tanzania kuifundisha Simba, naijua klabu ya Simba na mazingira yake, wana mashabiki wengi wenye mapenzi na timu yao"
"Pale Wydad nilisaini miezi minne kwa sharti la kubeba ubingwa wa Afrika tukapoteza kwa Ahly, CR Belouizdad ni tofauti nilikataa kupangiwa timu na viongozi," alisema Sven
Moja ya sifa yaker kubwa ni msimamo na nidhamu ya kazi, pengine anaweza kuwa kocha sahihi wa kikosi hiki ambacho baadhi ya wachezaji wanatupiwa lawama kuwa hawajitumi



