Karume Boys yatwaa CECAFA U-15

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th November 2023


Karume Boys yatwaa CECAFA U-15

Timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 15 kutoka Zanzibar 'Karume Boys' imetwaa taji la michuano ya Cecafa U-15 mwaka 2023 iliyokuwa inafanyika nchini Uganda

Karume Boys imeshinda kwa mikwaju ya penalti 4-3 dhidi ya wenyeji Uganda baada ya kumalizika kwa dakika 90 wakifungana bao 1-1

Wakati nafasi ya pili ikienda kwa Uganda, nafasi ya tatu imeshikwa na Tanzania Bara baada ya kushinda bao 1-0 kwa Sudan Kusini


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.