Timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 15 kutoka Zanzibar 'Karume Boys' imetwaa taji la michuano ya Cecafa U-15 mwaka 2023 iliyokuwa inafanyika nchini Uganda
Karume Boys imeshinda kwa mikwaju ya penalti 4-3 dhidi ya wenyeji Uganda baada ya kumalizika kwa dakika 90 wakifungana bao 1-1
Wakati nafasi ya pili ikienda kwa Uganda, nafasi ya tatu imeshikwa na Tanzania Bara baada ya kushinda bao 1-0 kwa Sudan Kusini



