Klabu ya Simba inatarajiwa kumtangaza kocha wake mkuu wiki hii kwani mchakato wa kumpata kocha kocha huyo uko mwishoni
Taarifa za uhakika kutoka ndani ya uongozi wa Simba, zimebainisha kuwa kocha huyo atatangazwa kabla ya Simba kuikabili Asec Mimosas mchezo wa kwanza hatua ya makundi ligi ya mabingwa Jumamosi
Ni wazi kocha atakayetangazwa sio miongoni mwa wale waliokuwa wakitajwa awali ambao ni mkufunzi wa zamani wa USM Alger Abdelhak Benchikha na Sven Vandenbroeck kwani mahitaji yao hayakwendana na mipango ya Simba
Kocha Radhi Jaidi raia wa Tunisia ndiye anayeonekana kuwa katika nafasi nzuri ya kumrithi Robertinho licha ya kuwa Simba pia ilifanya mazungumzo na Fernando Da Cruz Mkufunzi raia wa Ufaransa aliyewahi kuinoa klabu ya FAR Rabat ya Morocco
Jaidi amewahi kucheza timu ya Taifa ya Tunisia akiwa ni mlinzi wa kati pia amewahi kuinoa klabu ya Esperance na kuipa taji la Super Cup
Kocha huyo mwenye leseni ya UEFA Pro, anapenda kutumia mfumo wa 4-3-3, mewahi pia kuwa Kocha Mkuu wa Hartford Athletic inayoshiriki Ligi ya Marekani (USL Championship) huku akiwa pia kocha msaidizi wa timu ya Cercle Brugge ya Ubelgiji kabla ya kutua Esperance ya Tunisia alioachana nao mwaka jana akitoka kuwapa taji la Super Cup kwa kuifunga CS Sfaxien



