Transfer - International

Tetesi za soka Ulaya, Jumanne Novemba 21 2023

Joel JJ By Joel JJ
21 Nov 2023
Tetesi za soka Ulaya, Jumanne Novemba 21 2023

Chelsea wanafikiria kumnunua mshambuliaji wa Brentford na England Ivan Toney, 27, kwa pesa nyingi katika kipindi cha dirisha la usajili la Januari. (Football.London)

Chelsea, Manchester City, Manchester United na Newcastle United zote zilituma wawakilishi kumtazama winga wa Napoli Khvicha Kvaratskhelia, 22, wakati wa kushindwa kwao 3-1 na Uhispania Jumapili. (90min)

Arsenal na Manchester United ni miongoni mwa vilabu vinavyotarajiwa kuonyesha nia ya kumnunua mshambuliaji wa Brazil Marcos Leonardo, 20, ambaye wakala wake anasema atataka kuondoka Santos Januari. (Evening Standard)

Mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 24, anasema "kutakuwa na wakati wa kuzungumza" kuhusu mustakabali wake wa Paris St-Germain anapojiandaa kuingia miezi ya mwisho ya mkataba wake na klabu hiyo ya Ligue 1. (Telefoot, via Mail)

Benfica hawana mpango wa kuingia kwenye mazungumzo juu ya kiungo wa kati wa Ureno Joao Neves, 19, ambaye amekuwa akifuatiliwa na Manchester United, akiwa na kipengele cha kumnunua cha £105m. (Fabrizio Romano)

Bayern Munich wanaweza kufikiria kumnunua beki wa kati wa Manchester United na Ufaransa Raphael Varane, 30. (Sky Germany - in German)

Liverpool haitakubali ofa kwa winga wa Colombia Luis Diaz, 26, licha ya ripoti nchini Uhispania kwamba wanaweza kuidhinisha makubaliano ya kubadilishana na Barcelona kumnunua mshambuliaji wa Brazil Raphinha, 26. (Football Insider)

Meneja wa Bayer Leverkusen Xabi Alonso hana kipengele cha kuuzwa katika mkataba wake kinachomruhusu kujiunga na moja ya timu zake za zamani, Mkurugenzi Mtendaji wa klabu hiyo amesema, huku kukiwa na ripoti kwamba Mhispania huyo, 41, anaweza kuhamia Liverpool, Real Madrid au Bayern Munich. (Talksport)

Tottenham wako tayari kuwapa Roma £26m kwa ajili ya kiungo wa kati wa Italia Bryan Cristante, 28. (Tuttomercatoweb, via Teamtalk)

Tottenham hawajafurahishwa na madai ya Everton kwamba kukataa kwao kulipa pauni milioni 80 kumnunua mshambuliaji wa Brazil Richarlison, 26, kulisababisha The Toffees kukiuka kanuni za matumizi ya fedha za Premier League. (Mail)

Manchester United wanapanga kuchukua nafasi ya mkurugenzi wa soka John Murtough kama sehemu ya mabadiliko makubwa yatakayoambatana na uwekezaji wa Sir Jim Ratcliffe katika klabu hiyo. (MEN)

West Ham inasemekana kuwa na hasira huku kukiwa na hofu kwamba Michail Antonio amepata jeraha la muda mrefu akiwa na timu ya taifa ya Jamaica. (Telegraph - subscription required)

Mkurugenzi wa Girona Quique Carcel anasema klabu hiyo ingetamani kumsajili tena kiungo wa kati wa Uhispania Oriol Romeu, 32, kutoka Barcelona. (90min)

BBC

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
2h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
3h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
5h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
5h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
6h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
6h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
6h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
7h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
7h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
9h ago
READ MORE →