Baada ya mapumziko ya kalenda ya FIFA, Ligi Kuu ya NBC imerejea kwa kasi leo mechi mbili zikitarajiwa kupigwa
Matajiri wa Chamazi, Azam Fc watakuwa katika uwanja wao wa Azam Complex kuikabili Mtibwa Sugar katika mchezo utakaopigwa saa 12:30 jioni
Azam Fc wanashika nafasi ya pili katika msimamo wakiwa na alama 19 ushindi katika mchezo huo utawaogeza karibu na vinara Yanga wenye alama 24
Mtibwa Sugar inachechemea, inazihitaji alama tatu za leo ili kujiondoa chini ya msimamo wa ligi
Mchezo mwingine utakaopigwa leo ni derby ya kanda ya kati kati ya Dodoma Jiji dhidi ya Singida FG ambao utapigwa saa 3 usiku uwanja wa Jamhuri




