Azam Fc, Singida FG viwanjani Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 24th November 2023


Azam Fc, Singida FG viwanjani Ligi Kuu

Baada ya mapumziko ya kalenda ya FIFA, Ligi Kuu ya NBC imerejea kwa kasi leo mechi mbili zikitarajiwa kupigwa

Matajiri wa Chamazi, Azam Fc watakuwa katika uwanja wao wa Azam Complex kuikabili Mtibwa Sugar katika mchezo utakaopigwa saa 12:30 jioni

Azam Fc wanashika nafasi ya pili katika msimamo wakiwa na alama 19 ushindi katika mchezo huo utawaogeza karibu na vinara Yanga wenye alama 24

Mtibwa Sugar inachechemea, inazihitaji alama tatu za leo ili kujiondoa chini ya msimamo wa ligi

Mchezo mwingine utakaopigwa leo ni derby ya kanda ya kati kati ya Dodoma Jiji dhidi ya Singida FG ambao utapigwa saa 3 usiku uwanja wa Jamhuri


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.