Simba inaanza kampeni ya hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa barani Afrika kwa mchezo dhidi ya Asec Mimosas ambao utapigwa saa 10 jioni katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Kueleka mchezo huo, jana usiku Wanamsimbazi wakapokea taarifa njema baada ya Kocha Abdelhak Benchikha kutangwa kuwa kocha mkuu akichukua nafasi ya Robertinho Oliveira aliyetimuliwa mwanzoni mwa mwezi huu
Huu ni mchezo muhimu kwa Simba kuanza vyema kampeni ya kuisaka nusu fainali ya ligi ya mabingwa
Rekodi zinaibabe Simba, kwani katika misimu minne mfululizo imeweza kutinga robo fainali huku ikitumia vyema uwanja wa nyumbani
Silaha kubwa ya Simba katika mechi hizi ni mashabiki wake, bila shaka wengi watajitokeza kuishangilia timu yao hasa baada ya uongozi kumtangaza kocha mpya
Rais wa heshima klabu ya Simba Bilionea Mohammed Dewji 'Mo' alipunguza bei ya viingilio Mzunguuko ambapo ni Tsh 3,000/- badala ya Tsh 5,000/- ya awali
Ni wazi hautakuwa mchezo mwepesi lakini kwa wachezaji wa Simba hii inapaswa kuwa nafasi yao kuonyesha kilichotokea mechi mbili zilizopita ni upepo mbaya tu ambao ulipita
Ushindi dhidi ya Asec leo utarejesha ari na morali ya Simba katika msimu ambao Wanamsimbazi wanataka kuona mataji yakirejea Mtaa wa Msimbazi



