Mchezo wa Ligi ya Mabingwa kati ya Simba dhidi ya Asec Mimosas umemalizika kwa matokeo ya sare ya bao 1-1
Jinamizi la sare katika michuano ya CAF limeendeleza kuiandama Simba msimu huu
Simba ilitangulia kufunga bao la kuongoza kupitia kwa mkwaju wa penati wa Saido Ntibazonkiza kwenye kipindi cha kwanza kabla ya Asec kurejea katika kipindi cha pili wakiwa bora na kufanikiwa kusawazisha bao hilo
Yatasemwa mengi lakini ni wazi Simba inamuhitaji mtaalam wa 'fitness' haraka sana kwani timu 'inakata moto' kwenye kipindi cha pili
Simba ilicheza kwa nidhamu kubwa kwenye kipindi cha kwanza lakini kasi waliyokuja nayo Asec katika kipindi cha pili ilikuwa tatizo kubwa





