Simba - Local

Simba katika mtihani mgumu dhidi ya Wydad

Joel JJ By Joel JJ
β€’
4 Dec 2023
Simba katika mtihani mgumu dhidi ya Wydad

Kocha Mkuu wa Simba Abdelhak Benchikha ana kibarua kizito cha kuwavusha Wekundu wa Msimbazi robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika

Simba inakabiliwa na dakika 180 ngumu dhidi ya Wydad Athletic ya Morocco katika mechi mbili ambazo zitaamua hatma ya wababe hao wa soka katika ukanda wa Afrika Mashariki na kati

Msimu uliopita Simba ilianza vibaya mechi mbili za hatua ya makundi ikipoteza zote lakini ilifanikiwa kufuzu robo fainali kwa kushinda mechi tatu

Msimu huu pia haijaanza vyema kwani imetoka sare mechi mbili za mwanzo na kukusanya alama mbili tu sasa ikishika nafasi ya tatu katika msimamo wa kundi B

Inakwenda kumenyana na Wydad iliyo katika mazingira magumu zaidi, ikiwa imepoteza mechi zote mbili za mwanzo

Mchezo wa kwanza utapigwa Disemba 09 huko Morocco na mchezo wa pili kupigwa Disemba 20 jijini Dar es salaam

Simba inahitaji angalau alama nne kutoka katika mechi hizi mbili ili kuweka hai matumaini ya kutinga robo fainali

Benchikha hakuwa na mwanzo mbaya katika majukumu yake na Simba licha ya timu yake kulazimishwa suluhu ya bila kufungana dhidi ya Jwaneng Galaxy siku ya Jumamosi

Simba ilionyesha mabadiliko makubwa katika mchezo huo ambao ilikuwa ugenini, ilitawala na kutengeneza nafasi nyingi za kufunga

Akiwa na uzoefu mkubwa katika mashindano ya CAF, hakuna shaka chini ya Benchikha, Simba inaweza kuvuka salama katika mechi dhidi ya Wydad

More Stories

Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizzima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
3h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
6h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
7h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
7h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
8h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
9h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
10h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
10h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
23h ago
READ MORE β†’