Jana Namungo Fc iliichapa Dodoma Jiji bao 1-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkaoni Lindi
Bao pekee la ushindi kwa Namungo Fc liliwekwa kimiani na kiungo mshambuliaji Pius Buswita
Buswita mpaka sasa ana jumla ya magoli manne (4) akiwa ndiye kinara wa magoli kwa Namungo FC akifuatiwa na Reliants Lusajo mwenye magoli mawili
Wanaoongoza kwa magoli kwenye NBC Premier League msimu huu ni Stephane Aziz Ki, Jean Baleke na Maxi Mpia Nzengeli ambao kila mmoja ana magoli saba
Namungo Fc wamesogea mpaka nafasi ya nane kwenye msimamo wa ligi wakikusanya alama 14