Uongozi wa Simba tayari umeanza mchakato wa maboresho ya kikosi takribani siku 12 zikisalia kabla ya dirisha dogo la usajili kufunguliwa (Disemba 16)
Imeezwa kuwa Simba imemnasa winga hatari wa Mtibwa Sugar Ladack Chasambi
Nyota huyo alikuwa akiwindwa na vigogo wote kutoka jijini Dar es salaam (Simba, Yanga na Azam Fc) lakini ni kama Simba imeshinda vita ya kumsajili
Chasambi amekuwa mchezaji tegemeo katika kikosi cha Mtibwa Sugar ambacho msimu huu kina mwendo wa kusuasua
Simba imeruhusiwa kuzungumza na mchezaji kukubaliana maslahi binafsi baada ya kuwa tayari imefikia makubaliano na Mtibwa Sugar
Chasambi atakuwa mchezaji wa kwanza kutua Msimbazi pale dirisha dogo litakapofunguliwa