Yanga yaifuata Medeama

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th December 2023


Yanga yaifuata Medeama

Kikosi cha Yanga leo JUmanne Desemba 5 alfajiri kimeanza safari kuelekea Ghana kwa ajili ya kupambania kupata pointi tatu muhimu katika mchezo unaofuata kwenye ligi ya mabingwa dhidi ya Medeama Fc

Baada ya kucheza mechi mbili ambazo ni dakika 180 imekusanya pointi moja pekee. Yanga ina kibarua cha kusaka ushindi dhidi ya Medeama Desemba 8

Kikosi kilichoondoka kimejumuisha wachezaji 24, wachezaji watatu wakibaki jijini Dar es salaam ambao ni Crispin Ngushi, Denis Nkane na Joyce Lomalisa

Nyota waliosafiri ni Dickson Job, Nickson Kibabage, Kouassi Yao, Kibwana Shomari, Khalid Aucho, Mudathir Yahya, Salum Abubakar, Pacome Zou-zoua na Jonas Mkude

Wengine ni Zawadi Mauya, Stephane Aziz Ki, Maxi Nzengeli,  Farid Mussa, Mahlatsi Makudubela na Jesus Moloko

Pia wamo Kennedy Musonda, Clement Mzize, Hafiz Konkoni, Djigui Diarra, Metacha Mnata, Aboutwalib Mshery, Ibrahiim Bacca na Bakari Mwamnyeto


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.