Kikosi cha Yanga leo JUmanne Desemba 5 alfajiri kimeanza safari kuelekea Ghana kwa ajili ya kupambania kupata pointi tatu muhimu katika mchezo unaofuata kwenye ligi ya mabingwa dhidi ya Medeama Fc
Baada ya kucheza mechi mbili ambazo ni dakika 180 imekusanya pointi moja pekee. Yanga ina kibarua cha kusaka ushindi dhidi ya Medeama Desemba 8
Kikosi kilichoondoka kimejumuisha wachezaji 24, wachezaji watatu wakibaki jijini Dar es salaam ambao ni Crispin Ngushi, Denis Nkane na Joyce Lomalisa
Nyota waliosafiri ni Dickson Job, Nickson Kibabage, Kouassi Yao, Kibwana Shomari, Khalid Aucho, Mudathir Yahya, Salum Abubakar, Pacome Zou-zoua na Jonas Mkude
Wengine ni Zawadi Mauya, Stephane Aziz Ki, Maxi Nzengeli, Farid Mussa, Mahlatsi Makudubela na Jesus Moloko
Pia wamo Kennedy Musonda, Clement Mzize, Hafiz Konkoni, Djigui Diarra, Metacha Mnata, Aboutwalib Mshery, Ibrahiim Bacca na Bakari Mwamnyeto



