Simba safarini Morocco

Joel JJ By Joel JJ β€’ 5th December 2023


Simba safarini Morocco

Msafara unaojumuisha wachezaji 23 wa Simba, umeondoka saa 9 Alasiri leo kuelekea Morocco kwa ajili ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Wydad Athletic

Simba imeondoka nchini na Qatar Airways ambapo watasafiri mpaka Qatar ambako wataunganisha ndege nyingine kuelekea Casablanca na baadae kuelekea Marakech

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ally amesena wanakwenda Morocco wakiwa na ari kubwa kwenda kusaka alama tatu ugenini

"Chini ya kocha Benchikha, fitness ya wachezaji wetu imeongezeka kwa kiwango cha hali ya juu, hili linatupa matumaini kuwa tuko katika njia sahihi ya kufikia ubora ambao kila mmoja anataka kuuona"

"Wapinzani wetu katika kundi kila mmoja amevuna alama tatu kutoka kwa Wydad hili linatupa mtihani mgumu nasi kuona tunakwenda kuvuna chochote ugenini," alisema Ahmed


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.