Msafara unaojumuisha wachezaji 23 wa Simba, umeondoka saa 9 Alasiri leo kuelekea Morocco kwa ajili ya mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Wydad Athletic
Simba imeondoka nchini na Qatar Airways ambapo watasafiri mpaka Qatar ambako wataunganisha ndege nyingine kuelekea Casablanca na baadae kuelekea Marakech
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ally amesena wanakwenda Morocco wakiwa na ari kubwa kwenda kusaka alama tatu ugenini
"Chini ya kocha Benchikha, fitness ya wachezaji wetu imeongezeka kwa kiwango cha hali ya juu, hili linatupa matumaini kuwa tuko katika njia sahihi ya kufikia ubora ambao kila mmoja anataka kuuona"
"Wapinzani wetu katika kundi kila mmoja amevuna alama tatu kutoka kwa Wydad hili linatupa mtihani mgumu nasi kuona tunakwenda kuvuna chochote ugenini," alisema Ahmed













