Simba yaja na mkakati wa maboresho dirisha dogo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th December 2023


Simba yaja na mkakati wa maboresho dirisha dogo

Dirisha dogo la usajili linatarajiwa kufunguliwa wiki ijayo ambapo Simba imeanza mapema michakato ya maboresho ya kikosi chake

Kinda Ladack Chasambi kutoka Mtibwa Sugar anatajwa kuwa usajili wa kwanza ambapo Disemba 16 nyota huenda akaanza rasmi maisha yake Msimbazi

Taarifa kutoka ndani ya uongozi wa Simba zimedokeza kuwa takribani nyota watano wanaweza kuongezwa, uongozi unasubiri ripoti ya mwisho ya kocha Abdelhak Benchikha ambaye anatumia mechi za ligi ya mabingwa kufanya tathmini

Tayari Simba imewapa taarifa baadhi ya wachezaji kuwa wako huru kusaka timu na ruksa kuondoka pale dirisha litakapofunguliwa

Miongoni mwa wachezaji hao, ametajwa nahodha John Bocco ambaye kwa sasa ni kama ameshaondolewa kwenye mipango ya timu

Bocco ni mmoja wa wachezaji waandamizi katika kikosi cha Simba akidumu Msimbazi kwa takribani misimu saba

Bocco alitwaa mataji manne ya ligi mfululizo kuanzia msimu wake wa kwanza 2017/2018 hadi 2021/2022 pia kwa nyakati tofauti amekuwa mshambuliaji kinara akiibuka mfungaji bora wa ligi msimu wa 2020/2021 (mabao 16)


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.