Kocha Mkuu wa Simba Abdelhak Benchikha amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Wydad ambao utapigwa kesho Jumamosi huko Marrakesh, Morocco
Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari kueleke mchezo huo, Benchikha amesema anatambua hautakuwa mchezo rahisi lakini kutokana na umuhimu wake wanahitaji kupambana kuwania ushindi
Benchikha amesema anawafahamu vyema Wydad Athletic, ana imani vijana wake watakuwa bora katika mchezo huo
"Hii ni mechi nyingine ngumu tuliyokuja kucheza huku ugenini tukiwa na lengo la kutafuta ushindi"
"Nawafahamu Wydad, hii sio mara ya kwanza kukutana nao, wana timu nzuri ila naamini tuko tayari na tutakuwa bora dhidi yao," alisema Benchikha
Mchezo huo utapigwa kesho Jumamosi saa 4 usiku kwa saa za Morocco