Mtanange dume kati ya Medeama dhidi ya Yanga uliopigwa uwanja wa Baba Yara huko Ghana umemalizika kwa matokeo ya sare ya bao 1-1
Medeama walitangulia kufunga kupitia mkwaju wa penati kwenye dakika ya 27 kupitia kwa Jonathan Sowah kabla ya Pacome Zouzoua kusawazsha kwenye dakika ya 36
Ulikuwa mchezo wa wazi timu zikishambuliana kwa zamu, Yanga ikipoteza nafasi kadhaa adimu
Alama moja ugenini ina thamani kubwa kwa Yanga kwani Wananchi watahitaji kushinda mchezo unaofuata dhidi ya Medeama utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa ili kusogea juu kwenye msimamo
Aidha Al Ahly nayo imelazimishwa suluhu ya bila kufungana dhidi ya CR Belouizdad huko Misri
Matokeo hayo yanafanya kila timu kwenye kundi D iwe na nafasi ya kusonga mbele
Al Ahly wanaendelea kuongoza wakiwa na alama 5 wakifuatiwa na CR Belouizdad yenye alama nne sawa na Medeama. Yanga inashika nafasi ya nne ikiwa na alama mbili








