Simba - Local

Simba ugenini dhidi ya Wydad leo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
9 Dec 2023
Simba ugenini dhidi ya Wydad leo

Mnyama Simba Sc yuko mawindoni Morocco ambapo leo majira ya saa 4 usiku atashuka dimbani huko Marrakesh kuikabili Wydad Athletic katika mchezo wa ligi ya mabingwa barani Afrika, raundi ya tatu kundi B

Mchezo mwingine muhimu kwa Simba kuwania alama tatu ili kuweka hai matumaini ya kufuzu robob fainali

Hata hivyo ni mchezo ambao utahitaji wachezaji kujitoa kwa jasho na damu ili kuhakikisha malengo yanatimia

Wydad wamepoteza mechi zote mbili za awali, leo wataingia uwanjani wakiwa na dhamira ya kuzisaka alama tatu katika uwanja wao wa nyumbani

Ni mechi ya kuamua hatma yao, ni wazi utakuwa mchezo wenye presha kubwa lakini Simba ina uzoefu wa mechi za aina hii

Msimu uliopita timu hizi zilikutana hatua ya robo fainali Simba ikiwa na faida ya ushindi wa bao 1-0 waliopata kwenye mchezo wa kwanza

Mchezo ukamalizika kwa Wydad kushinda 1-0 na hivyo changamoto ya mikwaju ya penati ikatumika kuamua mshindi na Wydad kutinga nusu fainali

Kocha Mkuu wa Simba Abdelhak Benchikha ana uzoefu na soka la Morocco hivyo anafahamu ni namna gani leo kikosi chake kinapaswa kucheza ili kuhakikisha hawapotezi mchezo

Simba inahitaji ushindi katika mchezo huo lakini pia hata alama moja itakuwa na faida kuelekea mchezo wa marudiano ambao utapigwa Disemba 19 jijini Dar es salaam

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
3h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
3h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
4h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
5h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
5h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
6h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
7h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
20h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
20h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
21h ago
READ MORE β†’