Yanga - Local

Yanga kulipa gharama za uharibifu dimba la Mkapa

Joel JJ By Joel JJ
β€’
11 Dec 2023
Yanga kulipa gharama za uharibifu dimba la Mkapa

Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo imewasilisha malalamiko rasmi kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) kuwataka Yanga SC kugharamia uharibifu uliofanyika kwenye mchezo wao dhidi ya Al Ahly

Barua ya Wizara inasema, Wizara ilitoa kibali cha kufanyika kwa mchezo wa kimataifa kati ya Yanga SC (Tanzania) dhidi ya Al-Ahly (Misri) katika Uwanja wa Benjamin Mkapa uliofanyika Desemba 2

Hata hivyo, Wizara imepokea Malalamiko kutoka kwa Uongozi wa uwanja ambapo mashabiki wa Yanga SC wanalalamikiwa kwa kuwasha fataki wakati mchezo ukiendelea na kusababisha vurugu zilizopelekea baadhi ya viti kung'olewa

Wizara inakemea vikali kitendo hiki na kuwataka Yanga SC mara moja kuwasiliana na uongozi wa Uwanja ili kubaini ukubwa wa tatizo na kuona namna bora ya kulitatua

Kwa barua hii, Wizara inawasilisha rasmi malalamiko haya kwa TFF kwa kuwa ndiye mdhamini wa vilabu hivi kwa maombi ya matumizi ya uwanja huu ili kuwajulisha Yanga SC kuwa inapaswa kugharamia matengenezo ya viti vilivyong'olewa na mashabiki wakati wa mchezo huu

Aidha kuwaonya mashabiki wao kuacha mara moja tabia hizi ili uendelea kustawisha michezo na kuulinda Uwanja wa Benjamin Mkapa.

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
48m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’