Mwamuzi Halil Umut Meler alikumbana na kipigo jana akipigwa sehemu mbalimbali za mwili akiumizwa zaidi jichoni katika mechi ya Ligi Kuu Uturuki kati ya Ankaragücü na Rizespor
Miongoni mwa waliompiga ni Rais wa timu ya Ankaragücü, Faruk Koca ambaye alitoka jukwaani kwenda kumshambulia mwamuzi huyo

Tayari Rais wa Uturuki amesimamisha ligi zote kuchezwa kufuatia vurugu hizo
Rais wa timu ya Ankaragücü, Faruk Koca tayari amekamatwa baada kuonekana katika picha za video akimtwanga ngumi ya jicho mwamuzi Umut
Mechi hiyo ilimalizika kwa sare ya bao 1-1



