Ligi Uturuki yasimamishwa kisa refa kupigwa

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th December 2023


Ligi Uturuki yasimamishwa kisa refa kupigwa

Mwamuzi Halil Umut Meler alikumbana na kipigo jana akipigwa sehemu mbalimbali za mwili akiumizwa zaidi jichoni katika mechi ya Ligi Kuu Uturuki kati ya Ankaragücü na Rizespor

Miongoni mwa waliompiga ni Rais wa timu ya Ankaragücü, Faruk Koca ambaye alitoka jukwaani kwenda kumshambulia mwamuzi huyo

Tayari Rais wa Uturuki amesimamisha ligi zote kuchezwa kufuatia vurugu hizo

Rais wa timu ya Ankaragücü, Faruk Koca tayari amekamatwa baada kuonekana katika picha za video akimtwanga ngumi ya jicho mwamuzi Umut

Mechi hiyo ilimalizika kwa sare ya bao 1-1


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.