Beki wa zamani wa Juventus Giorgio Chiellini ametangaza kustaafu soka leo,Jumanne, Desemba 12
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 39 alitumia misimu miwili iliyopita katika LAFC na alikuwa amedokeza hivi majuzi kwamba angeweza kustaafu baada ya mwisho wa msimu kwenye MLS
Timu yake ya LAFC ilipoteza Fainali ya Kombe la MLS Jumamosi usiku. Chiellini alifunga mabao 36 katika mechi 561 akiwa na Juventus, akishinda mataji tisa ya Serie A, matano ya Supercoppa Italiana na matano ya Coppa Italia
Pia alifika Fainali ya Ligi ya Mabingwa mara mbili, mnamo 2015 na 2017. Aliwahi kuwa nahodha wa Italia katika michuano ya Euro 2020, iliyoshinda na Azzurri kwenye Uwanja wa Wembley
Chiellini anaweza kurejea Juventus baada ya kumalizika kwa maisha yake ya uchezaji. Kaka yake Claudio tayari ni sehemu ya klau hiyo, akifanya kazi kama Mkuu wa Eneo la Next Gen
Beki huyo mashuhuri pia ameweka mlango wazi wa kufanya kazi katika MLS ili kuchangia maendeleo ya ligi hiyo