Simba Queens mabingwa Ngao ya Jamii

Joel JJ By Joel JJ β€’ 12th December 2023


Simba Queens mabingwa Ngao ya Jamii

Ni rasmi Simba Queens imetwaa Ngao ya Jamii kwa ushindi wa mikwaju ya penati dhidi ya JKT Queens katika mchezo wa fainali uliopigwa uwanja wa Azam Complex

Dakika 90 za mchezo huo zilimalizika kwa matokeo ya sare ya bao 1-1 na Simba Queens kushinda kwa penati 5-4

Stumai Abdallah alitangulia kuifungia JKT Queens bao la kuongoza kabla ya Dunai Bhobho kuisawazishia Simba Queens

Simba Queens ikaweka kambani mikwaju yote mitano ya penati wakati JKT Queens wakikosa mkwaju mmoja

Ni taji la kwanza kwa Simba Queens msimu huu kama ilivyo kwa kaka zao Simba Sc ambao walitwaa Ngao ya Jamii mkoani Tanga


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.