Man United yatupwa nje UEFA CL

Joel JJ By Joel JJ β€’ 13th December 2023


Man United yatupwa nje UEFA CL

Safari ya Manchester United katika ligi ya mabingwa Ulaya msimu huu ilifikia tamati mapema Jumanne usiku baada ya kupoteza nyumbani kwa Bayern Munich na kusababisha vijana wa Erik ten Hag kumaliza mkiani mwa Kundi A

Baada ya kuchukua pointi nne pekee katika mechi tano za mwanzo, United wakihitaji kushinda ili kuwa na nafasi yoyote ya kusalia kwenye michuano hiyo

Lakini kichapo cha 1-0 kiliwafanya The Red Devils kumaliza katika nafasi ya nne kwenye kundi la UCL kwa mara ya kwanza tangu 2005

Hii ilikuwa kampeni mbaya zaidi ya United kwenye Ligi ya Mabingwa kuwahi kutokea

Klabu ya Manchester ilikuwa haijawahi kupata chini ya pointi sita katika hatua ya makundi

United pia iliweka rekodi mbaya ya kufungwa mabao 15 katika michezo yao sita - zaidi ya timu yoyote ya Ligi Kuu iliyowahi kufungwa kwenye kundi la UEFA CL


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.