Mtibwa Sugar - Local - Yanga

Katwila aandaa mkakati wa kuikabili Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
13 Dec 2023
Katwila aandaa mkakati wa kuikabili Yanga

Mtibwa Sugar itakuwa ugenini Jumamosi dhidi ya Yanga ambao wanarudi kwenye ligi baada ya kukosekana kwa muda kutokana na kubanwa na ratiba ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Katwila aliyejiunga na timu hiyo Oktoba, mwaka huu akitokea Ihefu FC, ameiongoza katika mechi sita na kushinda moja, ameliambia amesema kuwa wanaendelea na maandalizi kuhakikisha kikosi kinarudi kwenye ushindani bila kujali wanakutana na timu gani.

"Tutaingia kwa kuwaheshimu Yanga Jumamosi na siyo kuwaogopa tunacheza na timu yenye wachezaji 11 kama sisi na changamoto tunayoipitia ni kipindi cha mpito timu nyingi huwa zinapitia nyakati ngumu kama hizi matokeo haya hayanifurahishi, nimeandaa programu nyingine za mazoezi na kuwapa wachezaji muda zaidi wa mazoezi wa kuongeza viwango vyao," alisema

Kocha huyo alisema anataka kuiona Mtibwa Sugar ikiendelea kushiriki Ligi Kuu na kupanda juu katika msimamo. Mtibwa Sugar inaburuza mkia ikiwa na pointi tano baada ya kushuka dimbani mara 12.

Kocha huyo aliiongoza Mtibwa Sugar kupata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Geita Gold kabla ya kufungwa bao 1-0 na KMC kisha kupoteza 2-1 ilipocheza na JKT Tanzania na kukubali kipigo cha mabao 5-0 dhidi ya Azam FC huku ikikubali kufungwa mabao 2-1 na Tabora United kisha kuchapwa bao 1-0 na Namungo

Wakati yuko Ihefu Fc, Katwila aliwaongoza walima mpunga hao kupata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Yanga na sasa anakutana tena na Wananchi akiwa na Mtibwa Sugar

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
6h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
6h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
7h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
10h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
14h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
14h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
15h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
16h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
16h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
17h ago
READ MORE β†’