Simba - Local - Transfer

Simba kushusha kiungo mkabaji

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Dec 2023
Simba kushusha kiungo mkabaji

Kocha Mkuu wa Simba Abdelhak Benchikha anaanza 'project' ya kukisuka upya kikosi cha Simba katika dirisha dogo la usajili kazi ambayo atakwenda kuikamilisha katika usajili wa dirisha kubwa mwezi Juni/Julai

Imeelezwa wachezaji ambao atawasajili kwenye dirisha dogo ni wale ambao wanahitaji haraka ili kumaliza changamoto katika baadhi ya maeneo lakini kiuhalisia ni kuwa Simba itahitaji maboresho makubwa zaidi baadae

Eneo la kiungo mkabaji limekuwa wimbo wa Simba, licha ya usajili wa Fabrice Ngoma ambaye hata Benchikha alimwagia sifa kuwa antimiza vyema majukumu yake uwanjani, kilio cha kiungo mkabaji hakijamalizika

Simba inahusishwa kumuwania kiungo wa Kimataifa wa Chad Eric Mbangossoum mwenye umri wa miaka 23 anayeitumikia klabu ya Union Touarga ya Morocco, nchi ambayo Benchikha amewahi kufanya kazi katika klabu za Mouloudia d'Oujda, Difaa El Jadida, Raja Casablanca na RS Berkane kabla ya kujiunga na USM Alger

Hata hivyo kumpata Mbangossoum, Simba itahitaji kuvunja mkataba wake wenye thamani ya karibu Milioni 600. Huyu ni mchezaji ambaye Simba inaweza kumtumia hata kwenye michuano ya ligi ya mabingwa kama itafanikiwa kufuzu hatua ya robo fainali

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
31m ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
10h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
10h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
11h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
18h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
19h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
20h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
20h ago
READ MORE β†’