Yanga - Local - Mtibwa

Kamwe awaalika mashabiki wa Yanga Azam Complex

Joel JJ By Joel JJ
β€’
14 Dec 2023
Kamwe awaalika mashabiki wa Yanga Azam Complex

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Yanga Ali Kamwe amewaalika mashabiki wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi uwanja wa Azam Complex katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa Jumamosi

Kamwe amesema baada ya kushuhudia mazoezi ya Yanga kwa siku tatu yakifanyika katika uwanja wa Avic Town, amejiridhisha wachezaji wako tayari na wanautaka kwelikweli mchezo huo

Aidha Kamwe amesema malengo ya Yanga ni kufunga mwaka 2023 kibabe kwa kushinda mechi zote za ligi watakazocheza mwezi huu Disemba

"Nawaambia mashabiki wetu waje kwa wingi uwanja wa Azam Complex siku ya Jumamosi, tumewaandalia burudani ya soka itakayoambatana na magoli mengi"

"Mwananchi hakikisha Jumamosi unamaliza shughuli zako mapema ili uwahi Azam Complex kwani uwanja huu tunafahamu haubebi mashabiki wengi"

"Ari ya timu ni kubwa, wachezaji wako tayari nadhani Jumamosi mashabiki watashuhudia burudani nyingine ya aina yake kutoka kwa timu yao," alitamba Kamwe

Yanga imekuwa na rekodi nzuri katika mechi walizocheza dhidi ya Mtibwa Sugar katika misimu ya karibuni

Yanga imeshinda mechi sita zilizopita dhidi ya Mtibwa Sugar pasipo kuruhusu bao

Ikicheza katika uwanja wa Azam Complex msimu huu, Yanga imeshinda mechi zote zikiwemo za Ligi Kuu na hatua ya awali Ligi ya Mabingwa

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’