Vurugu zaiponza Singida FG

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th December 2023


Vurugu zaiponza Singida FG

Kamati ya uendeshaji na usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPLB), imeitoza faini ya sh1 milioni Singida Fountain Gate kwa kosa la kuvamia Uwanja wa Liti wakati wa mazoezi ya mwisho ya Coastal Union siku moja kabla ya mchezo baina ya timu hizo na kusababisha vurugu

Mbali na klabu kupigwa faini pia kamati imewatoza faini baadhi ya wachezaji pamoja na benchi la ufundi la Singida

Waliopigwa faini ni kipa Beno Kakolanya aliyefungiwa kucheza mechi tatu na faini ya Sh1 milioni kwa kumtolea lugha chafu kiongozi wa Coastal Union, Juma kindo

Kocha msaidizi wa timu hiyo, Thabo Senong amefungiwa mechi tatu na faini ya sh1 milioni na Deus Kaseke na Hamad Waziri wametozwa faini ya Sh500,000 kwa kushiriki vurugu hizo na kuwatolea lugha mbaya viongozi wa Coastal.

Kwa upande wa Coastal, mchezaji Roland Beakou ametozwa faini ya Sh500,000 kwa kosa la kumwaga kimiminika katika mstari wa katikati ya uwanja baada ya ukaguzi wa kitendo kilichotafsiriwa kama imani za kishirikina.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.