Simba yaichapa Kagera Sugar 3-0

Joel JJ By Joel JJ β€’ 15th December 2023


Simba yaichapa Kagera Sugar 3-0

Alama zote tatu zimebaki Msimbazi baada ya Simba kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Kagera Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC uliopigwa uwanja wa Uhuru

Ulikuwa ushindi wa kwanza kwa Kocha Abdelhak Benchikha ambaye leo ameiongoza Simba katika mchezo wake wa kwanza kwenye ligi

Simba iliuanza mchezo taratibu hata hivyo ilikwenda mapumziko ikiwa mbele kwa bao 1-0 lililofungwa na Sadio Ntibazonkiza kupitia mkwaju wa penati baada ya Ntibazonkiza mwenyewe kufanyiwa madhambi ndanii ya eneo la hatari

Simba iliongeza kasi ya mashambulizi kwenye kipindi cha pili ilikuwa ni suala la mabao mangapi Simba yatafungwa

Baada ya kosakosa nyingi Sadio Kanoute aliyetumika kama kiungo wa ushambuliaji leo akafunga bao la pili kwenye dakika ya 74 akiunganisha krosi ya Mohammed Hussein

Nahodha John Bocco yawezekana mashabiki wamepoteza imani kwake lakini yeye ameendelea kuifanya kazi yake vyema kila anapopewa nafasi akifunga bao la tatu kwenye dakika za lala salama

Bocco amefunga mabao mawili msimu huu yote akiyafunga akitokea benchi

Ni alama tatu muhimu kwa Simba ambazo zinawapandisha mpaka nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 22

Aidha ni ushindi ambao utaweka saikolojia ya wachezaji sawa kuelekea mchezo wa ligi ya mabingwa dhidi ya Wydad utakaopigwa Jumanne katika uwanja wa Benjamin Mkapa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.