Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limebainisha kuwa baadhi ya mechi za Ligi Kuu Bara zitaanza kuamuriwa kwa usaidizi wa teknolojia ya video ya waamuzi (VAR)
Hiyo ni kufuatia uamuzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF), kuipa Tanzania vifaa vya VAR ambavyo vitafungwa katika baadhi ya viwanja
Akizungumza katika mkutano mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) unaofanyika Iringa, Rais wa shirikisho hilo amesema , Wallace Karia amesema wanaandaa utaratibu wa ufungwaji wa vifaa hivyo kwa kushirikiana na wadu
"Niwape habari njema kuwa tumepata VAR kutoka CAF na hii ni mwendelezo wa uhusiano mzuri na CAF. Wataalamu wameingia jana kutoa mafunzo. Itafungwa katika viwanja vyenye standard (ubora)"
"Kamati ya waamuzi kwa vile tumewapa jukumu la usimamizi mtasaidia katika mafunzo na uzuri tunaye mkufunzi wa waamuzi wa CAF, Leslie Liunda ambaye atakuwa mratibu wa hayo mafunzo," alisema
Karia amesema kuwa wanaangalia pia uwezekano wa VAR kufungwa katika Uwanja wa Amaan Zanzibar ikiwa ni katika kuhakikisha kwamba mchezo wa soka unaendelea kupata mafanikio hapa nchini