Klabu ya Wydad Athletic imetua Dar es Salaam tayari kuivaa Simba SC kwenye mchezo wa hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika Jumanne ya Desemba 19
Mchezo huo muhimu kwa kila timu, utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Wydad walishinda bao 1-0 mchezo wa kwanza dhidi ya Simba uliopigwa Morocco wiki iliyopita na kufikisha alama tatu wakisogea nafasi ya tatu kundi B
Simba inayoshika nafasi ya nne ikiwa na alama mbili itahitaji kushinda mchezo huo ili kuweka hai matumaini ya kutinga robo fainali