Yanga - Local

Huyu Aziz Ki ni zaidi ya Mayele

Joel JJ By Joel JJ
18 Dec 2023
Huyu Aziz Ki ni zaidi ya Mayele

Mabao mawili aliyofunga Stephane Aziz Ki katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mtibwa Sugar, yamemfanya kiungo mshambuliaji huyo kuweka rekodi ya aina yake msimu huu

Juzi Aziz Ki aliisaidia Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 4-1 katika mchezo wa Ligi Kuu uliopigwa uwanja wa Azam Complex, Chamazi

Nyota huyo wa Kimataifa kutoka Burkina Faso, amefikisha mabao 9 baada ya mechi 10 msimu huu akiongoza orodha ya wafungaji bora

Ki ameivunja rekodi ya Fiston Mayele ya msimu uliopita ambapo baada ya mechi 10 alikuwa amefunga mabao saba na kutoa pasi mbili za mabao. Ki amefunga mabao 9 pia akitoa pasi mbili za mabao

Aziz Ki amehitaji mechi 10 tu kufikia rekodi yake ya mabao 9 aliyofunga msimu uliopita

Gamondi amtabiria ufungaji bora

Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema nyota huyo kama ataendelea kuwa katika ubora alionao sasa, ni wazi ataibuka mfungaji bora msimu huu

"Mwanzoni mwa msimu nilimwambia Aziz Ki, ana kipaji na uwezo wake wa kupiga mashuti ni kitu tofauti, akitumia vyema kipaji na maarifa yake, atafunga mabao mengi"

"Amefunga mabao mawili (dhidi ya Mtibwa Sugar) lakini utaona nafasi nyingine alikosa, angeweza kufunga hata mabao manne"

"Kama ataendelea kucheza hivi, nadhani ana nafasi kubwa ya kuibuka mfungaji bora," alisema Gamondi

Wakati baadhi ya wachambuzi wakiiona Yanga ina changamoto kwenye safu ya ushambuliaji lakini ndio timu yenye kinara wa mabao mpaka sasa Aziz Ki ambaye takwimu zake ni bora kuliko hata takwimu za Mayele baada ya mechi 10 za kwanza za msimu

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
5h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
6h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
8h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
8h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
9h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
9h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
9h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
9h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
10h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
12h ago
READ MORE →