Simba - Local

Benchikha hana hofu na Wydad

Joel JJ By Joel JJ
18 Dec 2023
Benchikha hana hofu na Wydad

Kocha Mkuu wa Simba Abdelhak Benchikha ameendelea kukiandaa kikosi chake kuelekea mchezo muhimu wa ligi ya mabingwa dhidi ya Wydad ambao utapigwa kesho Jumanne katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Simba inahitaji kushinda mchezo huu ili kuweka hai matumaini ya kutinga robo fainali ya michuano hiyo. Hivyo huu ni mchezo ambao dakika zake 90 zitaamua hatma ya Simba katika michuano hiyo ambayo malengo yaliyowekwa msimu huu ni angalau kucheza nusu fainali

Jana Simba ilikamilisha mazoezi yake ya mwisho katika uwanja wa Benjamin Mkapa ambapo baada ya mazoezi hayo Benchikha aliwahakikishia Wanamsimbazi kuwa kikosi chake kiko tayari na watafurahi baada ya dakika 90 za mchezo huo

Benchikha alisema hakuna timu isiyofungika huku akiwataka mashabiki wa Simba kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu yao katika mchezo huo muhimu

"Hakuna timu isiyofungika, tuondoe mawazo hasi kichwani kwetu tutaingia uwanjani tukiwa kifua mbele na lengo likiwa ni kushinda. Tunawaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi kuipa nguvu timu yao naamini baada ya mechi tutafurahi kwa pamoja," alisema

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
4h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
5h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
7h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
7h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
8h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
8h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
9h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
9h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
9h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
11h ago
READ MORE →