Mnyamaaaaaaaaaa amefanya yake uwanja wa Benjamin Mkapa akiibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Wydad Casablanca katika mchezo wa ligi ya mabingwa barani Afrika
Huu ni ushindi wenye thamani kubwa kwa Wekundu wa Msimbazi kwani umerejesha katika nafasi nzuri ya kufuzu robo fainali ya michuano hiyo
Zilikuwa dakika mbili za maajabu kutoka kwa Willy Essomba Onana akifunga mabao yote katika dakika ya 36 na 38
Alifunga bao la kwanza kwa shuti la nje kidogo ya 18 baada ya kutengewa pasi murua kutoka kwa Kibu Denis
Dakika mbili baadae Onana akawainua Wanamsimbazi kwa mara nyingine akiweka kambani bao bora la mchezo huo baada ya kupasiana 1-2 na Mzamiru Yassin
Kwa hakika leo Onana alikuwa na jambo lake kwani aliwapa wakari mgumu walinzi wa Wydad. Huyu ndiye Onana ambaye Wanamsimbazi walikuwa wakimsubiri tangu msimu huu ulipoanza
Alipata majeraha kwenye kipindi kocha Abdelhak Benchikha akilazimika kumtoa nafasi yake kuingia Israel Mwenda
Benchikha alifanya mabadiliko zaidi kwenye kipindi cha pili yaliyokuwa na lengo la kulinda ushindi
Duchu, Khamis, Bocco wote waliingia kuhakikisha alama zote tatu zinabaki Msimbazi
Simba imechupa mpaka nafasi ya pili ikifikisha alama tano, ikiwa bado na mecho moja nyumbani dhidi ya Jwaneng Galaxy
Kimahesabu Simba inahitaji alama tisa tu kutinga robo fainali kwa maana ushindi dhidi ya Jwaneng na angalau sare dhidi ya Asec katika mchezo unaofuata ambao utapigwa huko Ivory Coast mwezi Februari 2024



