Azam - Local - Kagera

Azam Fc ni mwendo wa vipigo Ligi Kuu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
22 Dec 2023
Azam Fc ni mwendo wa vipigo Ligi Kuu

Timu ya Azam imeendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu Bara baada ya jana kuendeleza wimbi la ushindi wakiichapa Kagera Sugar mabao 4-0 katika mchezo uliopigwa Uwanja wa Kaitaba, Bukoba

Mabao ya Azam yalifungwa na Feisal Salum 'Fei Toto' dakika ya '9, Prince Dube dakika ya 11, Pascal Msindo dakika ya 45 na Alassane Diao dakika ya 84 na kuifanya timu hiyo kufikisha jumla ya pointi 31 katika michezo 13 iliyocheza hadi sasa

Pointi hizo 31 ilizonazo Azam zinaifanya kuendelea kujikita kileleni na kuiacha Yanga ambao ni mabingwa watetezi wa taji hilo ikiwa na 27 ingawa imecheza michezo 10 ambayo ni mitatu pungufu ya vinara hao kwa sasa wa Ligi Kuu Bara msimu huu

Baada ya kufunga bao katika mchezo huo, Fei Toto amefikisha jumla ya mabao manane ya Ligi Kuu Bara akiwa na kikosi hicho msimu huu akipitwa moja tu na kinara wa Yanga, Stephane Aziz KI anayeongoza akiwa amefunga tisa

Ushindi wa Azam unaifanya timu hiyo kufikisha jumla ya michezo sita mfululizo ya Ligi Kuu Bara bila ya kupoteza tangu mara ya mwisho ilipofungwa mabao 3-1, dhidi ya Namungo Oktoba 27, mwaka huu kwenye uwanja wake wa Azam Complex, Chamazi

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
2h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
2h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
3h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
4h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
4h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
5h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
19h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
20h ago
READ MORE β†’